Subscribe:

Ads 468x60px

Pages

Monday, January 25, 2016

KIKUNDI CHA HAPA KAZI –UKEREWE MABINGWA MBIO ZA MAKASIA 2016.



Mabingwa wa mbio za Balimi Boat Race 2016 wakishangilia mara baada ya kushinda mbio za kupiga makasia wakitumia dakika 34. Mashindano mbio za Makasia ni mara ya 16 yakidhaminiwa na TBL kupitia bia ya Balimi Extra Lager,ambayo yalishirikisha vikundi 15 vya mkoa wa kimechezo wa Ukerewe
Na Mwandishi wetu,UKEREWE
VIKUNDI vya Wazee wa Mamba (Wanauame)na Hapa Kati tu  ( Wanawake),vya mkoa wa Michezo wa Ukerewe, vimevunja rekodi ya mashindano ya mbio za Mitumbwi za Balimi Boat Race 2016 na kutwaa ubingwa na kujinyakulia vikombe medali za dhahabu na fedha taslimu sh.2.2.
 
Mashindano hayo yalifanyika juzi kwenye ufukwe wa Monarch hoteli wilayani Ukerewe, ambapo mgeni rasmi Mkuu wa wilaya hiyo, Josephat Mkirikiti alikabidhi zawadi kwa washindi wa mivhuano hiyo inayodhaminiwa na kampuni ya Bia nchini (TBL) kupitia bia ya Balimi Extra Lager.
 Bingwa wa mashindano hayo kwa upande wa wanaume, kikundi cha Wazee wa Mamba kilitumia dakika 31 kuweza kutwaa ubingwa huo na kukabidhiwa kombe,medali za dhahabu na fedha taslimu, sh.1.2 ,huku Kikundi cha Hapa Kazi tu kwa wanawake,kiling’ara kwa kushika nafasi ya kwanza, kikitumia dakika 39 na kukabidhiwa fedha taslimu sh. 1,000,000,medali za dhahabu na kombe. 
Nafasi ya pili kwa wapiga makasia hao kwa wanaume ilikwenda kwa kikundi cha Kama Ipo Ipo tu kwa kutumia dakika 34 na kujinyakulia kitita cha sh.1,000,000, kikundi cha Ya Mtoto  kilinyakua nafasi ya tatu baada ya kutumia dakika 35 na kulamb sh.800,000 na  nafasi ya nne ilinyakuliwa na kikundi cha Tuliochelewa ambacho kiliondoka na sh.600,000.
Vikundi vya Usipoteze muda, Nani Kaona,Maisha ni kutafuta ,Mbeya City, Hapa Kazi tu na Ole wenu,vilivyoshika nafasi ya tano hadi ya kumi,kila kimoja kilipata kifuta jasho cha sh.250,000.
Kwa upande wa wanawake,nafasi ya pili ilikwenda kwa kikundi Kaza Roho,ambacho kilitumia dakika 41 na kikapata sh.800,000, kikundi cha  tatu cha Kazi na Malengo, kilitumiaz dakika 43 na kubeba sh.600,000 na nafasi ya nne ilichukuliwa na kikundi cha Upendo na kuzawadiwa sh.400,000.
Hata hivyo katika mashindano hayo kikundi cha nahodha Yasinta kutoka Kirumba mtumbwi wazo ulipinduka na kuzama lakini baada ya kuokolewa walibadili mtumbwi na kuendelea mashindano na ukashika nafasi ya tisa.
Vikundi vitatu vy tabia Njema, Mtafuta cha Uvunguni na Eberneza vilivyoshika nafasi ya tano hadi ya saba walifutwa jasho kwa sh.200,000 kila kimoja, hata hivyo vikundi vitatu viliondolewa kwenye mashindano hayo baada ya kubainika vilishiri mashindano kama hayo kwenye mikoa ya Mara na Mwanza, kimoja kikikishika nafasi ya kwanza na kingine nafasi ya pili.
Akizungumza wakati akikabidhi zawadi, Mkuu wa Wilaya, Mkirikiti, alisema kampuni ya TBL isichoke kupeleka mashindano kama hayo wilayani humo kwa sababu wananchi wake wanapenda michezo na burudani.
“TBL niwapongeze mnafanya vizuri katika eneo la kodi,mmekuwa marafiki wa Uerewe sababu mmetufanya tuwe sehemu ya maisha yenu.Changamoto yenu mtuangalie katika sekta za afya na elimu (madawati).Mtusaidie hili la madawati na tupo tayari kuondoa vikwazo vinavyowakwaza  ili tuondokane na kero ya madawati,”alisema Mkirikiti.
Pia, aliipongeza kampuni hiyo kwa kuwaondoa washiriki (mamluki) waliokwisha shiriki mashindano hayo mikoa mingine,ambo walikuja kuchukua nafasi zizizo za kwao na katika eneo lisilo la kwao.
Aidha, Meneja Mauzo wa TBL Kanda ya Ziwa, Godwin Zacharia,alisema lengo la TBL kwa miaka 16 ya mashindano ya Balimi, ni kukuza utamaduni na michezo ukiwemo wa kupiga makasia .
Alisema, kutokana na kukubaliwa na jamii ya Kanda ya Ziwa,wataendelea kuyaboresha kwa kuongeza zawadi na washiri kila mwaka kwa sababu bado wana kiu na kuahidi kushughulikia changamoto ya washiriki bandia . 
                             
Aidha, Mwenyekiti wa Chama cha Mitumbwi Taifa-Tanzania Canoe Assocition,(TCA) Richard Mgabo alisema kuwa, akiwa mwasisi wa mashindano ya makasia,anafarijika kuona mchezo huo ambao haukuwepo nchini, ukipata mashabiki na kuzidi kupendwa na wananchi wa kada mbalimbali na kuishukuru TBL kwa udhamini wao tangu yaanzishwe.
 Mashindano hayo Balimi Boat Race  yamefikisha umri wa miaka 16 tangu yaanzishwe mwaka 2000, kwa udhamini wa TBL kupitia kinywaji chake cha bia ya Balimi Extra Lager,ambapo mwaka huu Ukerewe yamefanyika kwa hadhi ya kimkoa baada ya wilaya hiyo kupewa hadhi ya mkoa.Fainali ya mwisho itafanyika Januari 30, mkoani Geita.

Saturday, January 16, 2016

Norwegian oil fund blacklists China's ZTE Corporation

 
Norway’s sovereign wealth fund has divested one of the world’s largest telecommunications companies over allegations of corruption and bribery.
The NOK7.1trn (€742bn) Government Pension Fund Global’s Council on Ethics last year investigated ZTE Corporation, listed on the Shenzhen and Hong Kong stock exchanges, over concerns it was responsible for gross corruption, as defined by the fund’s own exclusion guidelines.
In a statement, the fund’s manager, Norges Bank Investment Management, said its executive committee felt it was inappropriate to exercise its ownership rights to bring about change and instead opted to divest its stake worth NOK85m, accounting for just 0.15% in voting rights.
The Council’s report from June last year noted the company had been sent a draft version of its report but had not commented in the findings, which listed allegations of corruption in 18 countries.

Kampuni ya Huawei yatoa toleo jipya


Nevada.
KAMPUNI ya Huawei Consumer Business Group imezindua aina mpya ya simu za kisasa ya Huawei Mate 8.
Uzinduzi huo wa simu ulifanyika Las Vegas Marekani na kuhudhuriwa na viongozi wa juu wa Kampuni hiyo Duniani.
Mkuu wa Biashara wa Kampuni hiyo, Kavin Ho alisema Huawei Mate 8 ni simu yenye uwezo mkubwa wa kurahisisha mawasiliano ikiwa na betri linalodumu muda mrefu.
Alisema wameamua kuzindua simu hiyo ya kisasa ikiwa ni mwendelezo wa kampuni yao kutoa bidhaa bora kwa wateja wao na kukuza soko.
Alisema kuwa watumiaji wa simu hiyo wanaweza kutumia simu hiyo katika shughuli zao mbalimbali za kikazi na kufanya ufanisiwake kwani teknolojia iliyotumika katika utengenezaji ni ya hali juu.
“Unaweza kuitumia simu hii kufanya shughuli mbalimbali, kwa ufanisi wa hali ya juu,ina kasi na ufanisi mkubwa na betri lake likidumu kwa muda mrefu,” alisema Ho.
Alifafanua kuwa wameamua kutoa simu hiyo kwa kuzingatia hali halisi  ya kukua kwa kasi ya sekta ya mawasiliano.

Wednesday, July 15, 2015

KENICE KUKUTANISHA MIKOA SANA KATIKA BONANZA LA POOL NANENANE


Mratibu wa Nanenane Kenice Pool Bonanza 2015 (88 Kenice Pool Bonanza 2015), Michael Machellah(kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa kutangaza rasmi Bonanza hilo litakalofanyika jijini Dar es Saalaa.Katikati ni Meneka wa Kampuni ya KENICE Tanzania, Eustace Masaki na Mwenyekiti wa waamuzi wa mchezo wa Pool Taifa,  Hashimu Shaweji.
 
 
 
 
Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya kutengeneza meza za mchezo Pool ya KENICE imetangaza kudhamini Bonanza la mchezo wa Pool utakaoshirikisha Mikoa saba katika kusherehekea Sikukuu ya nanenane lijulikanalo kama “88 Kenice Pool Bonanza 2015.
Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja wa Kampuni ya Kenice Tanzania Limited, Bwana Eustace John Masaki alisema lengo la kufanya Bonanza hili ni kuendelea kuunga mkono mchezo huu kwa pale ulipofikia  ukizingatia sisi ndio Mabingwa wa kutengeneza Meza zinazotumika katika mchezo huu hivyo tumeona  ni jambo jema na ni sehemu ya pekee ya kukutanisha Vijana ambao ndio wachezaji wakuu wa mchezo huu wakabadilishana mawazo kwa njia ya mchezo wa Pool kuliko kuwaacha wakizagaa vijiweni.
Alisema Masaki, tutambue mchezo wa Pool ni michezo kama michezo mingine na ukizingatia michezo ni furaha,michezo ni afya na michezo ni ajira inayomfanya mtu yeyote kupiga hatua katika maisha ukianzia na sisi kama Kampuni bila wachezaji wa pool huko mitaani, hakuna wa kumuuzia hizi meza za pool tunazozalisha kila siku ambapo itapelekea wafanyakazi tulionao kukosa ajira.Hivyo tunakila sababu za kuunga mkono mchezo huu kuhakikisha unakua na unafaidisha jamii.
Masaki alisema zaidi  jumla ya  Sh.Mil.6 tumetenga kwa ajili ya Bonanza hili katika kusherehekea sikukuu ya nane nane kwa mwaka 2015.
Masaki alizitaja zawadi za Bonanza hilo kuwa Bingwa atajinyakulia Meza ya Pool ya kisasa kutoka Kenice yenye thamani ya Shilingi 2,000 000/= pamoja na pesa taslimu Shilingi 300,000/=
Mshindi wa pili atajinyakulia pesa taslimu Shilingi 500,000/=,mshindi wa tatu 300,000/= na wa nne 100,000/=.
Patakuwa na ushindani wamchezaji  mmoja mmoja (Singles) ambapo Bingwa atajinyakulia zawadi ya pesa taslimu Shilingi 200,000/=,mshindi wa pili 100,000/=,wa tatu 50,000/= na wane 30,000/=.
Nae mratibu wa Bonanza hilo Bwana Michael Machellah alisema  Bonanza hilo litaanza Agosti 7,8 na kumalizika 9,2015 katika Ukumbi wa CCM Mwinjuma Mwananyamala jijini Dar es Salaam kwa kushilikisha vilabu vyote vya mikoa ya kimichezo ya Ilala,Temeke,Kinondoni,Pwani, Morogoro, Iringa na Dodoma.
Machellah alimaliza kwa kutoa wito kwa vilabu vya mchezo wa Pool kujitokeza kwa wingi kuja kushiriki Bonanza hilo la sikukuu ya nanenane.
 

Monday, July 13, 2015

CCM YAANZA KUMTANGAZA MGOMBEA WAKE WA URAIS DK. JOHN MAGUFULI MJINI DODOMA.

 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi John Pombe Magufulu pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakiwasalimia wananchi waliojitokeza kwenye uwanja wa  Jamhuri mjini Dodoma  Dk. Magufuli akiwasalimia wananchi waliojitokeza kwa wingi kuja kumsalimia na kumuona mgombea huyo wa CCM.
Dk. Magufuli akisalimiana na wananchi
 Mgombea mwenza wa Dk. Magufuli, Samia Suluhu Hassan akiwasalimu wananchi wa Dodoma kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma
Dk. John Magufuli akizungumza na wakazi wa Dodoma ikiwa sehemu yake ya kwanza  kujitambulisha kwa wananchi baada ya kutangazwa kuwa mgombea rasmi wa CCM.

DK. JOHN MAGUFULI MGOMBEA RASMI WA URAIS KWA TIKETI YA CCM, AMTEUA SAMIAH SULUHU KUWA MGOMBEA MWENZA WAKE. 

Mwenyekiti wa CCM, Rais Jaaya Kikwete akionyesha kuwa mwenye furaha isiyo kifani baada ya Dk. John Magufui (kulia)  kutangazwa kuwa mshindi, na hivyo kupata ridhaa ya kupeperisha bendera ya CCM kaika uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwaka huu.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akimkaribisha jukwaani, Mke wa Dk. John Magufuli, Mama Janeth Magufuli
"Hili jembe" akisema Rais Kikwete wakati akiwa na Dk. John Maguli na Mama Janeth Magufuli baada ya matokeo ya uchaguzi wa kumpata mgombea wa CCM yaliyotangazwa na Spika wa Bunge Mama Anna Makinda leo mjini Dodoma
Rais Kikwete akionyesha zaidi furaha yake
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete (kushoto) akiwa na Mama Janeth Magufuli, huku Rais Kikwete akiendelea kufurahi
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimpongeza Dk. Magufuli
 
KABLA YA MATOKEO KUTANGAZWA
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiwasalimia wajumbe na wageni waalikwa baada ya kuwasili katika Ukumbi wa kisasa wa mikutano mjini Dodoma leo kwa ajili ya shughuli ya kutangazwa matokeo ya uchaguzi wa kumpata mgombea Urais kwa tiketi ya CCM ambao ulifanyika jana usiku.Kushoto ni Makamu wa Rais Dk. Mohammed Gharib Bilal, Makamu Mwenyekiti wa CCM Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein na kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete baada ya kuwasili katika Ukumbi wa kisasa wa mikutano mjini Dodoma leo kwa ajili ya shughuli ya kutangazwa matokeo ya uchaguzi wa kumpata mgombea Urais kwa tiketi ya CCM ambao ulifanyika jana usiku.Kushoto ni Makamu wa Rais Dk. Mohammed Gharib Bilal, Makamu Mwenyekiti wa CCM Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein na kulia ni Makamu Mwenyekiiti wa CCM Bara, Phlip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akihamasisha wajumbe  ukumbini wakati wakisubiri kutangazwa matokeo hayo
Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idi akisoma taaifa ya serikali, kabla ya kutangazwa matokeo hayo
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akijadiliana jambo na Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein wakati yakisubiriwa kutangazwa matokeo hayo. Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akieleza utekelezaji wa serikali wa ilani ya CCM wakati yakisubiriwa kutangazwa matokeo ya uchaguzi huo
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete na Katibu Mkuu wa CCM, Abdurahman Kinana wakitafakari mambo mbalimbali wakati wa kusubiri kutangazw amatokeo ya mgombewa urais kwa tiketi ya CCM katika uchagzi mkuu utakaofanyika mwaka huu
Mwimbaji Ali Star akiimba wimbo maalum wa CCM wakati wa shamrashamra a kusubiri matokeo hayo
Wajumbe na waalikwa wajikimwayamwaya ukumbini wakati wakisubiri matokeo hayo
Katibu Mkuu wa CCM mstaafu Mzee Wilson Mukaa akifuatilia hali ya mambo yalivyokuwa ukumbini wakati yakisubiriwa matokeo hayo
Spika wa Bunge Anna Makinda na Spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho, wakimkabidhi leo Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete matokeo ya uchaguzi wa mgombea Urais kwa tiketi ya CCM uliofanyika jana usiku
Spika wa Bunge Anna Makinda akitangaza matokeo hayo baada ya Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete kuyahakiki
Mgombea Urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka huu, kwa tiketi ya CCM Dk. John Magufuli (kushoto) wakati akisubiri kutangazwa kwa matokeo hayo
Walinzi wa usalama,  wakiwa wamemzunguka Dk. John Magufuli mara matokeo yalipoonyesha kuwa ameshinda na hivyo kuwa mgombea rasmi wa Urais kwa tiketi ya CCM leo
Dk. Magufuli akiwa 'amezongwa' na walinzi waliokuwa wakimpeleka jukwaani baada ya kuytangazwa kuwa ndiye mshindi
Dk. Magufuli akiwa 'amezongwa' na walinzi waliokuwa wakimpeleka jukwaani baada ya kuytangazwa kuwa ndiye mshindi
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akimsubiri kwa hamu Dk. John Magufuli wakati akipanda jukwaani
Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete akimkubatia kumpongeza Dk. Magufuli kwa kupata ushindi
Rais Kikwete akizidi kumpongeza Dk. Magufuli
"wewe ni jembe letu" akasema Rais Kikwete
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akimnadi kwa wajumbe Dk. Magufuli baada ya kutangazwa mshindi
Dk. Magufuli akimshuku Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein kwa jinsi Chama kilivyosimamia uchaguzi na kumalizika salama
Dk. Magufuli akimsalimia Makamu wa Rais Dk. Mohammed Gharib Bilal
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimpongeza Magufuli
Baadhi ya wadau ndani ya ukumbi wakati wa kutangazwa matokeo hayo.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimpongeza kwa furaha, Mama Janeth Magufuli
Aliyekuwa akiomba ridhaa ya CCM kuwania Urais, Mwigulu Nchemba naye akiungana na wadau kufurahia Dk. Magufuli kuibuka mshindi

BAADA YA MAGUFULI KUWA MGOMBEA RASMI KWA TIKETI YA CCM
 Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein akitoa maelezo alivyjipanga kuongoza tena mhulamwingie, kufuatia kuteuliwa tena kuwa mgombea wa Urais wa zanzibar kwa tiketi ya CCm katika uchaguzi utakaofanyika mwaka huu
 Aliyekuwa mgombea wa kupata ridhaa ya kugombea Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. Asha Rose Migiro akitoa shukrani zake, wakati wa kutangazwa matokeo ya mgombea urais kwa tiketi ya CCM na yeye kuibuka watatu kutokana na kupata kura chache Kushoto ni mumewe, Profesa Migiro
 Aliyekuwa mgombea wa kupata ridhaa ya kugombea Urais kwa tiketi ya CCM Balozi Amina Ally akitoa shukrani zake, wakati wa kutangazwa matokeo ya mgombea urais kwa tiketi ya CCM na yeye kuibuka wapili kutokana na kupata kura chachedhidi ya Dk. Magufuli
  Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM katika uchaguzi utakaofanyika mwaka huu, Dk. John Magufuli, akitoa maelezo yake alivyojipanga kuongoza nchi, baada ya kutangazwa kuwa mshindi wa kupata nafasi hiyo matokeo ya uchaguzi uliofanyika jana usiku yalipotangazwa leo
  Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM katika uchaguzi utakaofanyika mwaka huu, Dk. John Magufuli, akimnadi Mgombea wake mwenza, Samiah Suluhu, baada ya kutangazwa kuwa mshindi wa kupata nafasi hiyo matokeo ya uchaguzi uliofanyika jana usiku yalipotangazwa leo
 Samiah Suluhu akitafakari baada ya kuteuliwa na Dk. Magufuli kuwa mgombea wake mwenza
 Kisha akaonyesha furaha yake ya kuteuliwa huko kuwa mgombea mwenza
 Mama Janeth Magufuli akimpongeza samiah Suluhu. Kulia ni Mama Mwanamwema Shein
 Mama Salma Kikwete akiungana na Spika wa Bunge Mama Anna Makinda kumpongeza Samiah Suluhu
Mweneyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete akiufunga Mkutano Mkuu maalum, baada ya shughuli ya kutangaza matokeo ya mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM kumalizika leo, mjini Dodoma
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiwapongeza Dk.Magufuli na Samiah Suluhu baada ya kuufunga mkutano huo.
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete na baadhi ya viongozi wa meza kuu, wakiwa katika picha ya pamoja na Dk, Magufuli na Samiah Suluhu baada ya kufunga mkutano huo
 Rais Mstaafu Ali Hassani Mwinyi akiondoka ukumbini huku akiwa amemshika mkono Dk. Magufuli. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO-theNkoromo Blog